1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUrusi

Korea kaskazini yaikosoa Marekani kwa msaada wake, Ukraine

Tatu Karema
29 Aprili 2024

Korea Kaskazini imeikosoa Marekani kwa kusambaza makombora ya masafa marefu kwa Ukraine. Haya yameripotiwa leo Jumatatu na shirika la habari la serikali, KCNA lililonukuu taarifa ya wizara ya ulinzi ya nchi hiyo

https://p.dw.com/p/4fHOR
Kiongozi wa Korea Kaskazini , Kim Jong Un
Kiongozi wa Korea Kaskazini , Kim Jong UnPicha: Uncredited/KCNA/KNS/dpa/picture alliance

Hapo jana Jumapili, mkurugenzi wa idara ya mambo ya nje kuhusu masuala ya kijeshi katika wizara ya ulinzi wa kitaifa ya Korea Kaskazini, alinukuliwa katika taarifa akisema kuwa Marekani imesambaza kisiri makombora hayo kwa Ukraine na kuzua wasiwasi katika jamii ya kimataifa.

Korea Kaskazini yasema Marekani haiwezi kulishinda jeshi la Urusi

Mkurugenzi huyo ameongeza kuwa Marekani haiwezi kulishinda jeshi la Urusi na watu wake kwa aina yoyote ya silaha za kisasa ama msaada wa kijeshi.

Soma pia: Marekani yapitisha msaada wa dola bilioni 61 kwa Ukraine

Mnamo Aprili 24, afisa mmoja wa Marekani alisema kuwa katika wiki za hivi karibuni zaidi, nchi hiyo ilisafirisha kisiri makombora ya masafa marefu kuelekea Ukraine kwa matumizi katika vita vyake na Urusi.

Ushirikiano wa kijeshi kati ya Korea Kaskazini naUrusiunaimarika, hali inayoonekana na Marekani na washirika wake kama ongezeko la mvutano katika rasi ya Korea.